National News

MADEREVA VYOMBO VYA MOTO WATAKIWA KUTII SHERIA BARABARANI

Tarehe: 13 Sep, 2023


Katika kuzuia ajali za barabarani jeshi la polisi  Mkoani Kigoma limeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na  ukaguzi wa vyombo vya moto, utoaji wa elimu  kwa watumiaji wa  barabara wakiwemo madereva na watembea kwa miguu.

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Kigoma ACP Filemon Makungu amesema kuwa kwa kipindi cha tangu tarehe 1 Agosti, 2023  hadi tarehe 11 Septemba, 2023 jumla ya makosa 6,870 ya usalama barabarani yamekamatwa na kutozwa faini ambapo madereva (13) wamefikishwa mahakamani kwa makosa mbalimbali ya usalama barabarani ikiwa ni pamoja na mwendokasi, kuzidisha abiria na kupita magari mengine (wrong overtaking) katika maeneo hatarishi  hususani kwenye kona, pia madereva wawili (2) wamefungiwa leseni zao za udereva baada ya kukiuka sheria hizo

Aidha Jeshi la Polisi limewasihi madereva mkoani Kigoma na nchi nzima kwa ujumla kuendelea kutii  na kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kutokea kutokana na uzembe 

  • © Copyright - 2024
  • All rights reserved by - MainFm
  • Developed by - Mainfintech Lab