National News

MWINYI AKUTANA NA UONGOZI WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO KIMATAIFA

Tarehe: 11 Sep, 2023


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amekutana na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.January Y.Makamba, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Mbarouk Nassor

Pia amekutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Stephen Byabato na viongozi wengine wa Wizara hiyo waliofika Ikulu Zanzibar kujitambulisha baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan